Benki Kuu ya Tanzania imepewa tuzo maalum kwa kutambua mchango wake wa kipekee katika Mfuko Mkuu wa Serikali. Tuzo hiyo imetolewa tarehe 10 Juni 2025 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kukabidhiwa kwa Gavana wa BoT, Bw. Emmanuel Tutuba, katika hafla ya kupokea gawio na michango kutoka kwa Taasisi na Mashirika ya Umma na Kampuni ambazo Serikali ina hisa, iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.